Elimu ya Afya Kwa Jamii

FAHAMU KUHUSU HOMA YA EBOLA

FAHAMU KUHUSU HOMA YA EBOLA

Ugonjwa wa Homa ya Ebola ni ugonjwa wa hatari unaosababishwa na virusi vya ebola. Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa ya milipuko yajulikanayo kama homa za virusi vinavyo sababisha kutoka damu mwilini.


Kuna aina tano za virusi vinavyosababisha ugonjwa wa ebola kama ifuatavyo; Zaire ebola virus, Sudan ebolavirus,Taï Forest ebolavirus, na Bundibugyo ebolavirus).Hivi vinasababisha ugonjwa wa Homa ya Ebola kwa binadamu.Kirusi cha tano kinaitwa Reston ebolavirus ambacho husababisha ugonjwa wa Ebola kwa wanyama peke yake


Ugonjwa huu kwa asili huanzia kwa wanyama kama vile nyani, kima sokwe na popo. Ugonjwa wa homa ya ebola huambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu au binadamu kwa binadamu mwingine kwa njia ya haraka.


Jinsi ya ugonjwa wa homa ya ebola unavyoambukizwa toka kwa wanyama kwenda kwa binadamu


Binadamu anapata virusi vya ugonjwa wa homa ya Ebola kwa kula au kugusa viungo na majimaji ya wanyama pori wenye maambukizi ya ugonjwa huo.

Jinsi ya ugonjwa wa ebola unavyoambukizwa miongoni mwa jamii

  • Kugusa majimaji ya mwili kama vile damu, matapishi, jasho, mate, machozi, mkojo au


kinyesi kutoka kwa mtu aliyeambukizwa na ugonjwa huo

  • Kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyeku fa kwa ugonjwa wa ebola
  • Kugusa vyombo na nguo zilizotumiwa na mtu mwenye maambukizi ya ebola
  • Kutumia vifaa vilivyotumika kum hudumia mgonjwa wa homa ya Ebola kama vile Sindano au Nyembe
  • Kujamiana na mtu mwenye maambukizi ya virusi vya Ebola

Ugonjwa huu hauenezwi kwa njia ya Hewa,Maji au Chakula

 

      Dalili za ugonjwa wa homa ya ebola                      


Dalili za ugonjwa wa homa ya ebola huanza kujitokeza kwa mtu aliyeambukizwa na virusi hivi kuanzia siku 2 hadi 21 tangu kupata maambukizi. Dalili hizo ni pamoja na:

  • Homa kali
  • Kulegea kwa mwili
  • Maumivu ya misuli
  • Kuumwa kichwa na vidonda kooni
  • Mara nyingi dalili hizo hufuatiwa na kutapika, kuharisha na vipele vya ngozi
  • Kwa baadhi ya wagonjwa kutokwa na

virusi


damu hutoka sehemu za wazi za mwili kama vile kwenye macho, pua, masikio, mdomo na njia za haja ndogo na kubwa

    Matibabu                                                                 

Ugonjwa wa homa ya ebola hauna tiba

maalum wala chanjo, hata hivyo mgonjwa hutibiwa kulingana na dalili zitakazo ambatana na ugonjwa huo. Kuna uwezekano mkubwa wa kuepuka mgonjwa kupoteza maisha iwapo mgonjwa huyo hatawahi kupata huduma stahiki.

    Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa homa ya ebola Ugonjwa wa homa ya ebola unaweza

kuzuilika iwapo tutazingatia yafuatayo;


  • Epuka kugusa damu, matapishi, kamasi, mate, machozi, mkojo, kinyesi na majimaji yanayotoka kwenye mwili wa mtu mwenye dalili za ugonjwa wa homa ya ebola.
  • Epuka kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyekufa akiwa na dalili za ugonjwa wa homa ya ebola, toa taarifa kwenye kituo cha kutolea huduma za afya kwa ushauri.
  • Epuka kutumia sindano,Kiwembe,m kasi,nguo, matandiko, kitanda, godoro na vyombo vilivyotumika na mtu mwenye dalili za ugonjwa wa homa ya ebola


  • Epuka kukutana kimwili na mtu mwenye dalili za ugonjwa wa homa ya Ebola
  • Epuka kugusa wanyama kama vile popo, nyani sokwe, tumbili na swala au mizoga ya wanyama.
  • Zingatia ushauri na maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya na viongozi wa serikali.
  • Wahi kituo cha kutolea huduma za afya unapohisi mojawapo ya dalili za ugonjwa wa ebola
  • Toa taarifa mapema kwenye kituo cha huduma za afya au kwa viongozi wa serikali ya mtaa, kijiji au kata mara uonapo mtu mwenye dalili za ugon jwa wa ebola.







read more
FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA KISUKARI

Fahamu zaidi kuhusu ugonjwa wa Kisukari


Kisukari jina la kitaalamu hujulikana kama diabetes mellitus ni ugonjwa unaoonyesha viwango vikubwa vya sukari katika damu.

Ugonjwa wa kisukari ni mlolongo wa matatizo mwilini ya mda mrefu na mfupi kutokana na upungufu au kutoweza kutumika vizuri kwa kichocheo kinachoitwa insulin.

Insulin hutengenezwa na chembechembe zilizopo ndani ya kiungo cha kongosho. Miili yetu inahitaji insulin ili kuweza kutumia sukari tuliyonayo mwilini.

Sukari inatokana na chakula tunachokula kila siku na hutumika kwa kuupa nguvu mwilini.

Kwa kawaida sukari ikizidi, ile ziada inahifadhiwa katika ini kama mafuta. Mafuta hayo hubadilishwa kuwa sukari na kutumika wakati tukiwa na njaa kwa mda mrefu. Endapo kuna matatizo ya kutengeneza au kutumika kwa insulin, sukari mwilini huongezeka haraka na inamaanisha ugonjwa wa kisukari upo na dalili kuanza kuonekana kama zifuatazo.

  1. Kunywa maji mengi kuliko kawaida na kusikia kiu kila wakati.
  2.  Kwenda haja ndogo mara kwa mara. Watoto kukojoa kitandani.
  3. Kuwa dhaifu, kukosa nguvu na kujisikia mchovu kila wakati.
  4.  Kupungua uzito au kukonda licha ya kula vizuri.
  5.  Kusikia njaa kila wakati na kula sana.
  6.  Wanawake kuwashwa ukeni.
  7.  Kutoona vizuri.
  8.  Kupungua nguvu za kiume au hamu ya kujamiiana kwa wanawake.
  9. Ganzi, kuchomwachomwa au kutohisi unapoguswa sehemu za miguu, viganja na vidole
  10. Miguu kuoza na hata kupata gangrini.
  11.  Kukaukwa na ngozi na pia kupata aina ya ngazi katika miguu.
  12.  Vidonda au majeraha sehemu yoyote ya mwili kutopona haraka.
  13.  Majipu mwilini.
  14. Kukojoa mkojo ambao mara baada ya dakika chache hujaliwa na sisimizi.

Mara uonapo dalili hizi wahi mapema hospitali kupima ugonjwa wa Kisukari kwa ni miongoni mwa magonjwa yanayochukua muda mrefu kutibika endapo mgonjwa atachelewa kupata matibabu, pia ni miongoni mwa magonjwa ambayo huua kwa kasi zaidi nchini.

Kuna nmana tofauti ya kujizuia kupata ugonjwa wa kisukari, ikiwemo kufanya mazoezi, kula vyakula vyenye afya kama matunda, mboga za majani na kula vyakula vyenye virutubisho vyote, na mwisho kujitahidi kupima kiwango chako cha sukari mwilini ili kujua kama kuna uwezekano wa kupata ugonjwa huo ili hatua zaidi zichukuliwe.

VIEPUKE VYAKULA HIVI VINASABABISHA KISUKARI...

UTAFITI mbalimbali uliokwishafanywa unaonyesha kuwa ugonjwa wa KISUKARI (DIABETES MELLITUS) unatokana na vyakula tunavyokula kila siku katika maisha yetu. Katika siku za hivi karibuni, ongezeko la ugonjwa huu limekuwa kubwa kwa sababau vyakula vinavyosababisha ugonjwa huu, ndivyo vinavyoliwa sana kuliko vile vinavyozuia.

Wiki hii tunawaletea orodha ya vyakula vinavyoaminika kuongoza kwa kuwa chanzo cha ugonjwa huu hatari:VYAKULA VYA KUKAANGA
Vyakula vingi vinavyotayarishwa kwa kukaangwa kwenye mafuta yenye moto mkali huwa na madhara kiafya na miongoni ma madhara hayo ni pamoja na kusababisha kansa ya kwenye mfuko wa uzazi. Vyakula hivyo ni pamoja na chips na vyakula vingine vinavyopikwa kwa kukaangwa kwenye mafuta.VYAKULA VYENYE CHUMVI NYINGI
Vyakula vyenye chumvi nyingi vimebainika navyo kusababisha kansa. Vile vile inaelezwa kuwa chumvi huwa kama chakula kwa bakteria wa kansa tumboni. Kansa ya tumbo inadaiwa kuua watu wengi nchini Japan kutokana na jamii hiyo kupenda sana vyakula vyenye chumvi nyingi. Miongoni mwa vyakula vyenye chumvi nyingi ni vile vya kusindika, kama vile nyama za makopo, maharage, n.kSUKARI
Matumizi mabaya ya sukari yanaelezwa kusababisha kansa. Kama tujuavyo, kuna aina mbalimbali za sukari lakini sukari hatari zaidi ni zile zinazowekwa kwenye vinywaji mbalimbali, zikiwemo soda, juisi za ladha ya matunda ambazo huwa na kiwango kingi cha ‘fructose’ ambayo inaelezwa kusababisha saratani ya kongosho.
Vile vile sukari kwa ujumla wake hairuhusiwi kutumiwa na mtu ambaye tayari amegundulika kuwa na kansa kwa sababu chakula cha chembechembe za saratani mara nyingi huwa ni sukari. Kwa matumizi mengine ya kawaida, sukari inatakiwa kutumiwa kwa kiwango kidogo sana katika vinywaji au vyakula tunavyotumia, tofauti na baadhai ya watu wanavyoweka sukari nyingi ili kupata utamu zaidi.NYAMA ILIYOIVA SANA
Upikaji wa nyama kwa muda mrefu na kwenye moto mkali (high temperatures) husababisha aina fulani ya kemikali inayojulikana kitaalamu kama ‘heterocyclic aromatic amines’. Utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na Chuo Kikuu cha Utah (University of Utah), umeonesha kwamba watu wanaopenda kula nyama zilizoiva sana, wako hatarini zaidi kupatwa na saratani ya njia ya haja kubwa (Rectal Cancer). Hivyo inashauriwa unapopika nyama, usipike kwenye moto mkali na kuiva kupita kiasi.

POMBE
Unywaji wa pombe kupita kiasi nao unaelezwa kusababisha aina nyingi ya saratani, kwa wake kwa waume. Aina ya saratani zinazodaiwa kusababishwa na pombe ni pamoja na satarani ya mdomo, ini, utumbo na koromeo, ambazo ndizo zinazoua watu wengi hivi sasa nchini Marekani.NYAMA NA MAFUTA
Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Havard nchini Marekani, umegundua kwamba watu wanaopenda kula nyama kila siku wako hatarini kupatwa na saratani ya utumbo kuliko wale wanaokula mara moja moja. Pia baadhi ya mafuta ya wanyama na yale yanayowekwa kwenye ‘baga’ au ‘cheese’ huweza kusababisha kansa.
Vile vile ulaji wa vyakula vilivyotengenezwa kwa kuchanganya na nyama zilizosindikwa au kuhifadhiwa kwa matumizi ya muda mrefu husababisha saratani pia. Vyakula hivyo ni pamoja na ‘soseji’ ambazo hupendwa na watu wengi. Pia mikate ya nyama ‘hot dogs’ nayo ni chanzo cha magonjwa ya saratani.

VYAKULA VYA UNGA MWEUPE
Vyakula vyote vinavyopikwa kutokana na unga uliokobolewa na kuondolewa virutubisho vyake vyote na kuwa mweupe, vinaelezwa kuchangia magonjwa ya saratani kwa kiasi kikubwa. Vyakula hivyo ni pamoja na ‘donati’ (doughnuts), maandazi, mkate mweupe, n.k
Mwisho, licha ya kuepuka ulaji wa vyakula vilivyotajwa hapo juu, unatakiwa kuzingatia ulaji wa vyakula asilia vitokanavyo na mimea, mboga za majani na matunda kwa wingi kila siku. Utaona kwamba adui mkubwa wa afya zetu ni vyakula vyote vya kusindika na vile vya kutengenezwa viwandani au vile ambavyo wakati wa utayarisjaji wake huondolewa virutubisho vyake vya asili.
read more
FAHAMU KUHUSU KIFUA KIKUU

Ufahamu Ugonjwa wa Kifua Kikuu (Tuberculosis)

Ugonjwa wa kifua kikuu ni kati ya magonjwa matatu yanayotokea sana kwa watu masikini duniani (Disease of poverty). Magonjwa mengine katika jamii ya disease of poverty ni malaria na Ukimwi (AIDS). Ugonjwa wa kifua kikuu huathiri asilimia 98 ya watu katika nchi zinazoendelea, ukimwi asilimia 95 na malaria asilimia 90.

Magonjwa haya matatu husababisha vifo asilimia 10 ya idadi ya watu wote duniani kwa ujumla, ambapo inakisiwa watu wote duniani ni 6.91 bilioni kulingana na kituo cha kuhesabu watu cha Marekani ( US Census Bureau).

Kwa Tanzania, watu 120,191 hukisiwa kuwa na ugonjwa wa kifua kikuu kila mwaka, hii ni kutokana na taarifa ya shirika la USAID ya mwaka 2007. Kati ya watu hawa (120,191), 56,233 ni wale wanaogundulika kuwa na ugonjwa huu kupitia makohozi yaani sputum smear positive (SS+ ). Vifo vinavyotokana na ugonjwa wa kifua kikuu ni 32,000 kila mwaka nchini Tanzania.

Tanzania ni ya 15 kati ya nchi 22 ambazo zimeathiriwa sana na ugonjwa huu. Kati ya asilimia 50 ya wagonjwa wa kifua kikuu waliopimwa virusi vya ukimwi mwaka 2007, inakadiriwa ugonjwa wa ukimwi huathiri asilimia 47 ya wagonjwa wote wa kifua kikuu. Ugonjwa sugu wa kifua kikuu (Multidrug resistant tuberculosis) huathiri watu 1,300 nchini Tanzania kulingana na taarifa ya mwaka 2007.

Je, ugonjwa wa kifua kikuu husababishwa na nini?

Ugonjwa wa kifua kikuu, husababishwa na bakteria wanaojulikana kama Mycobacteria tuberculosis. Kuna aina nyingi za jamii ya Mycobacterium kama Mycobacteria tuberculosis (husababisha kifua kikuu), Mycobacteria leprae (husababisha ugonjwa wa ukoma), Mycobacteria bovis (huathiri ngombe na binadamu), Mycobacteria afrikanum na kadhalika.

Ugonjwa wa kifua kikuu unaweza kuathiri mapafu, mishipa ya fahamu, mifupa, mfumo wa mzunguko wa damu, ngozi, viunganishi vya mifupa (joints) na lymphatic system.

Mycobacteria bovis ambayo huathiri ngombe, inaweza kuambukiza binadamu kama atakula bidhaa zinazotokana na maziwa ya ngombe ambayo yameathirika na bakteria hawa kama vile siagi, mtindi, maziwa yenyewe, cheese, ice cream nk. Aina hii ya bakteria huathiri mapafu, tezi (lymph nodes), tumbo na sehemu nyingine za mwili.

Ni asilimia 10 tu ya watu walio na bakteria wa Mycobacteria tuberculosis ambao hawapati ugonjwa huu wa kifua kikuu.

Mycobacteria tuberculosis waligundulika kwa mara ya kwanza na mwanasayansi kutoka ujerumani anayeitwa Robert Koch mwaka 1882 na kupewa tuzo ya amani ya Nobel kwa ugunduzi wake huu.

Kuna aina ngapi za ugonjwa wa kifua kikuu?

Kuna aina kuu tatu za ugonjwa wa kifua kikuu

  • Kifua kikuu kinachosababisha madhara (Active tuberculosis) – Hutokea pale ambapo bakteria waliopo mwilini wapo hai na kinga ya mwili imeshindwa kuwadhibiti hawa bakteria wasisababishe madhara. Watu hawa wanaweza kumuambukiza mtu yoyote kifua kikuu kwa njia ya kuvuta pumzi kama watakohoa, kutema mate, kupiga chafya, kupiga kelele iwapo watafanya vitendo hivi karibu na watu wasio na ugonjwa huu.
  • Ugonjwa usiosababisha madhara (Inactive tuberculosis) – Kwa kitaalamu pia unaitwa latent TB. Hapa inaamaanisha ya kwamba kinga ya mwili imeweza kuwadhibiti bakteria na kuwafanya kushindwa kusababisha madhara. Mtu mwenye latent TB, hana dalili za ugonjwa huu, hajisikii mgonjwa na hawezi kuambukiza mtu mwingine ugonjwa wa kifua kikuu. Aina hii inaweza kujirudia baadae na kuathri sehemu ya juu ya mapafu na hivyo kusababisha kikohozi cha kawaida ambacho baadae huongezeka na kusababisha kikohozi cha damu au makohozi, homa, kupungua hamu ya kula, kupungua uzito bila sababu ya msingi na kutokwa jasho kwa wingi kuliko kawaida wakati wa usiku.
  • Ugonjwa uliosambaa Mwilini (Milliary tuberculosis) – Hii hutokea pale ambapo kinga ya mwili imepungua na kusababisha ugonjwa wa kifua kikuu kuenea kupitia damu hadi sehemu nyingine za mwili kama mifupa, mishipa ya fahamu, ngozi, figo, kibofu cha mkojo, ngozi ya moyo (pericadium), mfumo wa uzazi, viunganishi vya mifupa (joints) na lymphatic system. Husababisha homa, kupungua hamu ya kula, kuchoka na kupungua uzito.

Vihatarishi vya ugonjwa wa kifua kikuu

Vihatarishi vya ugonjwa huu ni kama ifuatavyo

  • Kuzeeka
  • Unywaji pombe kupindukia
  • Kuishi sehemu zilizo na mrundikano wa watu kama mabweni, kambi za jeshi nk.
  • Magonjwa yanayoathiri kinga ya mwili kama Kisukari nk.
  • Wafanyakazi wa huduma ya afya
  • Ugonjwa wa HIV
  • Utapia mlo
  • Umaskini au hali duni ya kipato
  • Kuishi kwenye nyumba za jamii mfano nyumba za wazee
  • Wale wasio na makazi
  • Baadhi ya dawa – Dawa za ugonjwa wa maumivu ya mifupa (athritis)
  • Wasafiri au watalii kutoka nchi zilizo na idadi kubwa ya ugonjwa wa kifua kikuu.

Dalili na viashiria vya ugonjwa wa kifua kikuu

  • Kukohoa zaidi ya wiki 2-3 na kuongezeka kutoa makohozi

  • Kukohoa damu
  • Homa
  • Kupungua hamu ya kula
  • Kupungua uzito kwa asilimia 10 ya mwili.
  • Kutokwa na jasho kwa wingi wakati wa usiku
  • Uchovu
  • Maumivu makali ya kichwa
  • Maumivu ya kifua
  • Kupumua kwa shida

Vipimo vya kifua kikuu

  • Kipimo cha makohozi (Sputum for AFB) – Makohozi huchukuliwa kwa siku tatu mfululizo muda wa asubuhi na kupelekwa maabara kufanyiwa uchunguzi ili kuweza kugundua kama mtu ana TB. Kwa wale wagonjwa wasioweza kutoa makohozi au wale wenye TB ya tumbo basi hufanyiwa kipimo cha gastric lavage.
  • Picha ya X-ray ya kifua – TB ya mapafu huweza kugundulika kutumia kipimo hiki.
  • Kipimo cha kwenye ngozi – Tuberculin skin test (Mantoux test) – Hufanywa na daktari. Daktari huchoma dawa ya protein purified derivatives (PPD) kwenye ngozi ya mgonjwa, kama kutatokea uvimbe zaidi ya 5mm (0.2 in) baada ya masaa 48, basi mgonjwa huyo ana TB. Kipimo hiki kinaweza kutoa majibu ambayo si sahihi hasa kwa wale ambao wamepata chanjo ya ugonjwa wa kifua kikuu, wenye ugonjwa wa hodgkins lymphoma, sarcoidosis na hata utapia mlo. Majibu yake ni lazima yasomwe na daktari.
  • Kipimo cha PCR (Polymerase Chain Reaction assay) – Kipimo hiki kinahusisha utambuzi wa bakteria wanaosababisha kifua kikuu kupitia vina saba vyao (DNA of bacteria). Ni kipimo cha uhakika zaidi.
  • Kuotesha bakteria maabara (Bacteria culture) – Kipimo hiki huchukua muda mrefu na ni ghali.

Tiba ya kifua kikuu

Tiba ya kifua kikuu inahusiha matumizi ya dawa za kifua kikuu kwa muda wa miezi sita au tisa. Dawa hizi zinahusisha matumizi ya miezi 2 ya kwanza ya dawa aina ya isoniazid, rifampicin, pyrazinamide, na matumizi ya miezi 4 ya isoniazid, rifampicin na ethambutol au streptomycin. Dawa hizi hutolewa chini ya uangalizi yaani mgonjwa anakunywa chini ya uangalizi wa mhudumu wa afya (Directly Observe Treatment, short course). Tiba ya ugonjwa wa kifua kikuu inatolewa bure nchini kote Tanzania.

Upasuaji unaweza kufanyika kwenye mapafu kama dawa zimeshindwa kutibu kifua kikuu.

Jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa kifua kikuu

  • Chanjo ya ugonjwa wa kifua kikuu ipo na inasaidia kukinga TB (BCG Vaccine) na imeleta mafinikio katika kukabiliana na kifua kikuu. Kawaida hutolewa kwa watoto baada ya kuzaliwa.
  • Kuziba pua na mdomo kwa kitambaa (mask) ili kujikinga na kifua kikuu.
  • Kufanya mazoezi mara kwa mara ili kuimarisha kinga ya mwili.
  • Kupata usingizi wa kutosha.
  • Kwenda hospitali kufanya vipimo mara kwa mara. Inashauriwa kufanya kipimo cha ngozi angalau mara moja kwa mwaka.
  • Kuimarisha kinga ya mwili kwa kula vyakula venye virutubisho vyote muhimu kwa afya bora.
  • Kutumia dawa aina ya isoniazid (INH) kwa wale walio kwenye hatari ya kuambukizwa kifua kikuu.
  • Shirika la afya duniani (WHO) linapendekeza wagonjwa wa ukimwi (HIV) ambao wana Latent TB wapewe dawa ya isoniazid (INH) kama kinga dhidhi ya kifua kikuu kila inapohitajika.
  • Kuepuka mikusanyiko au mrundikano wa watu kama vile kwenye mabweni, kambi za jeshi, baa nk
  • Kuishi kwenye nyumba ambayo ina mfumo mzuri wa kuingiza na kutoa hewa yaani iwe na madirisha makubwa na ya kutosha.
read more
FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA HOMA YA INI

UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS) : MAMBO MUHIMU YA KUFAHAMU

Ini ni kiungo muhimu sana ndani ya miili yetu, hufanya kazi zaidi ya 500 ; moja ya kazi ni kuchuja na kuondoa sumu kutoka kwenye damu.

Kutokana na sababu mbalimbali kama pombe iliyopita kiasi, sumu kwenye damu au maambukizi; ini hupata shida na kuvimba na kushindwa kufanya kazi vizuri. Hii hali huitwa HOMA YA INI au HEPATITIS.

Katika maeneo yetu, bara la Afrika maambukizi ya virusi wa Homa ya ini ndio sababu kuu ya shida kwenye ini. Virusi vya Homa ya ini vipo vya aina 5 (A,B,C,D,E).

Aina mbili za virusi (B na C ) ndio sababu kuu za ugonjwa wa homa ya ini na husambaa kupitia damu na majimaji ya mwili.

Homa ya ini ni sawa janga linaloua kimya kimya kulingana na takwimu za vifo za dunia inakadiriwa Kirusi cha homa ya ini aina ya B pekee huua watu 600,000 hivi kila mwaka.

Kwa wastani zaidi ya watu bilioni mbili, yaani, asilimia 33 hivi ya watu wote ulimwenguni, wameambukizwa virusi vya HBV, na wengi wao hupona baada ya miezi michache. Watu milioni 350 hivi huendelea kuwa na virusi hivyo mwilini, wengi huishi bila dalili na kuendelea kuambukiza watu wengine

NAMNA GANI UNAWEZA KUAMBUKIZWA VIRUSI VYA HOMA YA INI (B NA C)…….?

Virusi vya homa ya ini B na C husambaa kupitia damu, shahawa au maji maji mengine ya mwili.

Virusi hivi vina uwezo wa kusambaa na kuambukiza mtu mara 100 zaidi ya virusi vya UKIMWI.

Njia hizi husambaza virusi hivi vya homa ya ini..:

Kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto
➡️Mama aliye na maambukizi ya Hepatitis B kumuambukiza mtoto wakati wa kujifungua, iwapo hamna juhudi za kitiba za kuzuia maambukizi kuna uwezekano hadi asilimia 90 kwa mama kumuambukiza mtoto.

Kufanya mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini

Kuchangia vifaa vyenye ncha Kali kama sindano hasa kwa watumia madawa ya kulevya au wachora tattoo, miswaki

Kuongezewa damu ambayo ina maambukizi ya homa ya ini.

Virusi vya homa ya ini vinaweza ishi nje ya mwili kwa muda mrefu…

Tafiti zinaonyesha virusi vya homa ya ini vinaweza ishi nje ya mwili hadi kwa muda wa siku 7, bado vikiwa na uwezo wa kuambukiza mtu. Tafiti zimeonyesha hata iliyokauka huwa na uwezo wa kuambukiza virusi hivi.


NB : Iwapo kuna damu imemwagika inatakiwa isafishwe na chlorine au spirit ili kuua virusi

NANI YUPO KATIKA HATARI ZAIDI YA KUPATA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA HOMA YA INI?

° Watoto wachanga waliozaliwa na mama aliye na maambukizi ya virusi vya homa ya ini

° Watu wanaofanya biashara ya ngono

°Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume wenzao

°Watu wanaojidunga dawa za kulevya

° Mtu mwenye mpenzi ambaye anaishi na maambukizi ya virusi vya homa ya ini

° Wafanyakazi wa sekta ya Afya

° Watu wa familia wenye ndugu anayeishi na maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini

°Wagonjwa wa figo wanaotumia huduma za kusafisha damu (dialysis)

UGONJWA WA VIRUSI VYA HOMA YA INI HUJA NA DALILI MBALIMBALI…..

Dalili za muda mfupi (acute hepatitis)

➡️ Dalili hizi za mwanzo hutokea ndani ya miezi 6 baada kuambukizwa virusi vya homa ya ini, hutokea kwa baadhi ya watu hazitokei kwa kila mtu.

Mgonjwa mwenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini hujiskia kuumwa

Hupoteza hamu ya kula

Kichefuchefu na kutapika

Mwili kuuma

Mkojo kuwa na rangi iliyokolea kama Coca-Cola

Kupata manjano kwenye macho, vinganja vya mikono/kucha au mwili mzima.

Kuna kundi dogo la wagonjwa wa homa ya ini hupata ugonjwa mkali wa ini na kusababisha ini kushindwa kabisa kufanya kazi pia huweza kusababisha kifo. Hii hatua huitwa “fulminant liver failure”.

Maambukizi ya kudumu ya virusi vya Homa ya ini (chronic hepatitis)

Watu wenye maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini mara nyingi huwa hawana dalili, kadri muda unavyoenda virusi husababisha ini kusinyaa (cirrhosis) na kushindwa kufanya kazi vyema.

Pia Maambukizi ya virusi vya homa ya ini huchangia pia kupata Saratani ya ini.

Kwa nini ni muhimu kupima ili kujua kama una maambukizi ya virusi vya homa ya ini? ….

Watu wengi huishi na maambukizi ya virusi vya homa ya ini bila kufahamu. Kwa kawaida katika kipindi fulani cha maisha mtu 1 kati ya watu 3 huambukizwa virusi vya homa ya ini. Baada ya kuambukizwa, kuna kundi la watu hubaki na maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini ambayo huwa hayana dalili yoyote na kuendelea kuua ini kimyakimya. Dalili huja kuonekana waziwazi miaka mingi baada ya mtu kuambukizwa. Huonekana wakati tayari ini limenyauka au lina kansa.

Hivyo Mtu aliye na maambukizi ya kudumu ya virusi vya homa ya ini aina B akianza matibabu mapema, anaweza kuzuia ini lake lisiharibike sana. Pia kwa wenye maambukizi ya virusi aina C matibabu ya dawa wiki 12 humaliza virusi vyote.

NANI ANAHITAJI KUPIMWA MAAMBUKIZI YA HOMA YA INI?

Watu kutoka makundi yafuatayo ni sharti kupimwa kama wana maambukizi ya virusi wa homa ya ini……

Watu wanaoishi kwenye maeneo yenye maambukizi ya virusi vya homa ya ini kwa zaidi ya asilimia 2. -Tanzania ni moja ya nchi zenye kiwango cha maambukizi ya virusi vya homa ya ini kwa wastani wa 5% hivyo watanzania wote ni muhimu kupima

Watu wote wanaotumia dawa za kulevya na kujidunga

Wafanyakazi katika sekta ya afya

Watu wote wanaoishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI

Watu wote ndani ya familia wanaoshi na ndugu aliyeambukizwa virusi vya homa ya ini

Watu wote wanaotumia dawa za kufubaza kinga ya mwili (immunosuppressive therapy)

Watu wote wenye ugonjwa wa figo wanahitaji kuanza dialysis

Kina mama wajawazito wote

Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume wenzao.

UGONJWA WA HOMA YA INI HUWA NA MATOKEO MABAYA…..

Kwa wastani watu 25 kati ya 100 walioambukizwa virusi vya homa ya ini wakiwa watoto na 15 kati ya 100 waliopata maambukizi ya kudumu ya homa ya ini baada ya utoto hufariki wakiwa na umri mdogo kwa ugonjwa wa ini (ini kushindwa kufanya kazi) au saratani ya ini.

CHANJO YA DHIDI YA VIRUSI VYA HOMA YA INI

Chanjo dhidi ya homa ya ini hutolewa kwa watoto wote kama ilivyo kwenye mpango wa chanjo wa Taifa, pia hutolewa kwa watu wazima ambao hawajawahi kupata chanjo.

Chanjo hutolewa kwa njia ya sindano, ambapo huwa ni sindano 3; sindano ya kwanza hutolewa baada ya kupimwa kujua kama hauna maambukizi tayari, sindano ya pili hutolewa baada ya mwezi mmoja na sindano ya 3 baada ya miezi 6.

Makundi ambayo ni lazima kupatiwa chanjo ya homa ya ini

Watoto wote

Watu wote wanaotumia dawa za kulevya na kujifungua

Watu wote wanaoishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI

Watu wote ndani ya familia wanaoshi na ndugu aliyeambukizwa virusi vya homa ya ini

Watu wote wanaotumia dawa za kufubaza kinga ya mwili (immunosuppressive therapy)

Wanaume wanaofanya mapenzi na wanaume wenzao

Watu wote wanaoufanya biashara ya ngono

Watu wote ambao wana mpenzi zaidi ya mmoja ndani ya miezi 6

Watu wenye maradhi ya kudumu ya ini

Watu wengine wote wanahitaji KUJIKINGA dhidi ya virusi vya homa ya ini


read more
FAHAMU KUHUSU SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI

Ijue Saratani Ya Shingo Ya Kizazi

SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI  NI NINI?

Saratani ya shingo ya kizazi ni saratani ambayo hutokana na mabadiliko ya mfumo wa chembechembe au cells zilizoko katika shingo ya kizazi. Mabadiliko haya hupelekea chembe chembe hizo kushamiri na kuzaliana kwa kasi kinyume na mpangilio wa maumbile.Saratani ya Shingo ya kizazi yasemekana kuwa ni saratani inayoongoza kwa kusababisha vifo vya wanawake katika nchi zinazoendelea. Ripoti ya 2012 ya shirika la afya duniani 'WHO' imesema kati ya matukio 75,000 ya waathirika wa saratani ya kizazi barani Afrika, 50,000 walifariki dunia. 

NINI KINACHOSABISHA SARATANI YA SHINGO YA UZAZI?

Ripoti za utafiti wa kisayansi zimeafiki kuwa asilimia 99% ya saratani za shingo ya kizazi hutokana na maambukizi ya virusi vya 'Human Papillomavirus' au HPV vilivyoko katika jamii ya papilloma. Baadhi ya virusi hivi vyenye aina zaidi ya mia moja huambukizwa kwa njia ya kujamiana.

BAADHI YA MAMBO YANAYOONGEZA HATARI ZA KUPATA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI

  • Kushiriki tendo ndoa katika umri mdogo au chini ya miaka 18. 
  • Kuwa na wenzi tofauti au mwenzi aliye na wapenzi tofauti.
  • Utumiaji wa sigara kwani hupunguza nguvu ya kinga mwilini(impairs immune system).
  • Watu wenye kinga hafifu ya mwili au magojwa kama Ukimwi.
  • Uzazi wa mara kwa mara

BAADHI YA DALILI ZA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI

  • Kutokwa na majimaji au uchafu wenye harufu kali ukeni.
  • Kutokwa na damu ukeni mbali na siku za mwezi au baada ya tendo la ndoa.
  • Maumivu makali ya sehemu ya chini ya tumbo ( pelvic area).
  • Kuhisi maumivu makali wakati wa kujamiiana.
  • Kupungua kwa uzito wa mwili bila kukusudia.
  • Mkojo wenye matone ya damu


JE SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI HUTIBIKA?

Saratani ya shingo ya kizazi yaweza kutibika iwapo itagundulika mapema. PAP TEST (PAPANICOLAOUS TEST);Pap-Smear ni kipimo ambacho hutumika kuchunguza mabadiliko ya chembe zilizoko katika mlango wa kizazi ili kugundua mabadiliko yanayotokea katika chembe hizo na hivyo kuwahi kuyakabili mapema.

UMRI WA KUPATA PAP TEST

Test hii hushauriwa kwa wanamke wa umri wa miaka 21 hadi 65 na chini ya umri wa miaka 21 endapo ameingia katika tendo la ndoa kwa kipindi kisichopungua miaka 3. 

KUPUNGUZA HATARI ZASARATANI YA SHINGO YA KIZAZI

  • Pap tests.

 Waweza kupata Pap test mara 1 kwa mwaka au mara 1 kwa miaka 2- 3,hii itategemea ushauri wa daktari,umri,hali yako ya afya kwa ujumla, na majibu uliyoyapata katika testi zilizotangulia na mfumo    wako wa maisha. 

  • Pata HPV vaccine (hii yashauriwa kati ya umri wa miaka 12 hadi 26 chini ya mwongozo wa daktari) . 
  • Kuwa na mpenzi mmoja. 

           Mahusiano ya kimwili na mtu mmoja hupunguza hatari za maambukizi ya magojwa ya zinaa. 

  • Tumia kinga (condoms). Hii husaidia kupunguza maambukizi ya magojwa ya zinaa.
read more
FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA CORONA (COVID-19)

Hiki ni kirusi cha aina gani?

Corona ni jamii kubwa ya virusi vinavyosababisha maradhi kwa wanyama na binadamu. Kwa binadamu, jamii kadhaa za virusi vya Corona vinafahamika kusababisha maambukizi kwenye njia ya hewa na mfumo wa upumuaji.  Maradhi yaliyowahi kusababisha madhara makubwa kutokana na virusi vya Corona ni pamoja na MERS na SARS yaliyozuka mwanzoni mwa miaka ya 2000. Kirusi cha Corona kilichogundulika hivi karibuni kinasababisha ugonjwa unaofahamika kama COVID-19.

COVID-19 ni nini?

COVID-19 ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na virusi vya Corona. Virusi hivyo vipya havikuwa vikifahamika hapo kabla na sayansi ya tiba. Na vilianzia nchini China mwezi Disemba mwaka 2019.

Dalili za Corona ni zipi?

Dalili kuu za Corona ni pamoja na Homa kali, Uchovu na Kikohozi kikavu na zinatokea taratibu. Dalili kubwa na inayoweza kutia hofu, ni mtu kukosa pumzi. Lakini isikutishe, ni mtu 1 pekee kati ya watu 6 walioambukizwa virusi vya Corona hufikia dalili hiyo ya hatari. Na asilimia 80 ya walio na virusi hivyo hupata nafuu bila kuhitaji msaada wa matibabu.

Makundi yaliyo kwenye hatari zaidi ni yapi?

WHO inasema wazee na watu wenye magonjwa ya kudumu kama Shinikizo la Damu, Kisukari, Matatizo ya Figo ndiyo walio kwenye hatari zaidi ya kuathika pindi wanapopatwa na virusi vya Corona. Watu wa umri wa wastani na wenye afya imara wanaweza kupata virusi vya Corona na kupona bila kuhitaji matibabu.

Virusi vya Corona vinasambaa vipi?

Symbolbild Hände waschen (Imago Images/M. Westermann)

Watu wanaweza kupata Virusi vya Corona kutoka kwa watu walioambukizwa. Virusi vinaweza kusambaa kupitia maji maji kutoka kwenye pua au mdomo wa aliyeathirika. Iwapo mtu anagusa maji maji kama mafua, mate na makohozi ya mtu aliye na virusi na kisha kujigusa mdomo, macho na pua anaweza kupata virusi vya Corona.

Ninaweza kujikinga vipi na Virusi vya Corona?

  1. Nawa vizuri na kila wakati mikono yako kwa maji ya vuguvugu, sabuni au dawa za kuua vijijidudu kwa angalau sekunde 20.
  2. Kaa umbali wa angalau hatua mbili (2) kutoka mtu anayepiga chafya au kukohoa.
  3. Epuka kushika macho, pua na mdomo kwa mikono isiyo safi kwa sababu mikono hushika sehemu nyingi na ni rahisi kubeba vimelea vya maradhi.
  4. Hakikisha wewe, na walio karibu yako wanazingatia ustaarabu wa kuzuia pua na mdomo wakati wa kukohoa au kupiga chafya.
  5. Baki nyumbani ikiwa hujisikii vizuri. Iwapo una mafua makali, homa, kikohozi na kushindwa kuhema nenda hospitali kwa sababu huko wataalamu watakupatia msaada muhimu
  6. Epuka kuwa sehemu yenye msongamano, kama vyombo vya usafiri, maduka na maeneo yenye yenye mgandamizo wa hewa.
  7. Nunua kifunika mdomo na pua na kukikavaa ukiwa kwenye mikusanyiko.
  8. Fuatilia taarifa za afya na matangazo yake kuhusu virusi vya Corona.

Kwanini watu wanawekwa karantini?

Kwa ufupi neno Karantini linamaanisha kuwa chini ya uangalizi. Watu wenye dalili au wanaotokea maeneo yenye maambukizi makubwa ya virusi vya Corona hulazimikwa kuwekwa karantini (kutengwa na watu wengine) ili kufuatilia afya yao kwa karibu na kuzuia kueneza virusi. Ukiambiwa unapaswa kuwekwa Karantini, usiogope. Ni kwa ajili ya afya yako na wengine.

Virusi vya Corona vina tiba?

Hadi sasa hakuna tiba au chanjo dhidi ya virusi vya Corona lakini kwa sababu virusi hivyo vinaleta dalili mfano wa zile za mafua makali, mchanganyiko wa tiba unatumika kupunguza athari za virusi vya Corona.

Ninapaswa kuwa na hofu?

Hapana. Hupaswi kuogopa wala kuwa na hofu. Bali unapaswa kuchukua tahadhari. Kila mtu duniani yuko kwenye uwezekano wa kupata virusi vya Corona lakini kama tulivyokufahamisha, athari zake bado hazitishi.

Ni kweli watu weusi hawawezi kupata Corona?

Hapana, kama ilivyo kwa watu wa rangi na jamii zote sisi watu weusi pia tunaweza kuambukizwa virusi vya Corona. Mfano ni mgonjwa aliyegundulika Kenya.

read more
FAHAMU KUHUSU UGONJWA WA UVIKO 19 (COVID 19)

Mnamo Januari 2020 Shirika la Afya Duniani (WHO) lilitangaza mlipuko wa ugonjwa mpya wa virusi vya korona katika Mkoa wa Hubei, Uchina, kuwa suala la Hali ya Hatari ya Afya ya Umma Kimataifa kwa sababu ya uwezekano mkubwa wa Ugonjwa wa Virusi vya Korona vya mwaka 2019 (UVIKO-19) kuenea duniani kote. Kufikia Aprili 2 2020, wagonjwa zaidi ya 896, 450 wameambukizwa katika nchi zaidi ya 200, zaidi ya watu 45, 526 wamekufa kutokana na ugonjwa huo, lakini wengine 135,000 pia wametibiwa na kupona tangu kuzuka kwa ugonjwa huo. Katika Jumuiya ya Afrika Mashariki matukio ya ugonjwa huu wameripotiwa nchini Burundi, Kenya, Rwanda, Uganda na Tanzania. Watu wengi walioambukizwa huonyesha dalili zisizo kali na kiwango cha takribani 4% cha vifo ulimwenguni ni cha chini kikilinganishwa na magonjwa mengine ya kuambukiza yanayotokea ukanda huu kama vile VVU/UKIMWI, surua au Ebola. Janga hili  halijaathiri tu sekta ya afya, bali limeathiri uchumi kwa ujumla, ikiwa ni pamoja na biashara na utalii, ambazo ndio nguzo kuu za maisha katika ukanda huu.

Ili kufanikiwa katika kukabiliana na janga hili, makundi yote katika jamii yetu ikiwa ni pamoja na waajiri na wafanyabiashara – ni lazima yahusike na kushirikiana. Kirusi ambacho husababisha Ugonjwa wa Virusi vya Korona (UVIKO-19) ni cha aina mpya ambacho hakikuwa kimewahi kutokea kwa binadamu hadi ugonjwa huo ulipozuka mwaka wa 2019.

Virusi vya Korona (ViKo) ni kundi kubwa la virusi ambavyo kwa kawaida hupatikana kwa wanyama na husababisha maradhi hatari yanyohusiana na upumuaji kama vile Dalili za Upumuaji za Middle East (Middle East Respiratory Syndrome (MERS-CoV) na Dalili Kali na Hatari za Upumuaji (Severe Acute Respiratory Syndrome (SARS- CoV).

Virusi vya korona huambukizwa baina ya wanyama na watu. Uchunguzi wa kina ulibaini kuwa virusi vikali na hatari vya SARS-CoV viliambukizwa binadamu kutoka paka aina ya ngawa navyo virusi vya upumuaji vya MERS-CoV viliambukizwa binadamu kutoka ngamia wenye nundu moja. Kuna virusi vya korona vingine vinavyojulikana kuwa vinapatikana miongoni mwa wanyama bila kusababisha ugonjwa kwa binadamu.

read more