WATUMISHI WANAWAKE WA HOSPITALI YA SEKOUTOURE WATOA HUDUMA ZA VIPIMO BURE

Posted on: March 1st, 2023

Katika kuelekea kilele Cha maadhimisho ya siku ya Mwanamke Duniani Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekoutoure imeandaa kutoa huduma za vipimo vya magonjwa mbalimbali. 

Vipimo ambavyo vitatolewa ni pamoja na
✔️Kupima Homa ya Ini
✔️Shinikizo la Damu.
✔️Saratani ya Matiti na Mlango wa kizazi
✔️Upimaji wa VVU
✔️Uchangiaji Damu

Huduma hii imeanza tarehe 01/ 03 hadi atrehe 05/03/2023 katika viwanja vya Hospitali ya Rufaa ya mka wa Mwanza Sekou toure kuanzia saa moja na nusu asubuhi hadi saa kumi jioni.